14 February, 2007

NINI KINACHOWAFANYA WATU WAZAE IDADI FULANI YA WATOTO? JE NI UFAHARI, HULKA, DOLA, DINI AU UWEZO WA KIFEDHA?

Labda ndugu msomaji jiulize swali hilo. Kiasi cha majuma mwezi mmoja hivi uliyopita
nilionyesha jinsi gani kunakuwa na ongezeko la watoto wa mitaani. Na leo bado jicho langu limejikita zaidi mitaani na kuzimulika familia tofauti katika pande kuu nne za dunia.

China ni moja kati ya mataifa makubwa barani Asia na dunia kwa ujumla. Inakadiriwa kuwa na robo ya watu wote duniani, ambayo ni watu bilioni moja na nusu. Idadi hiyo ya watu, labda ingekuwa zaidi ya hapo kama serikali (dola) ya nchi hiyo isingeweka idadi ya mtoto mmja katika kila mwanandoa. Hivyo, wananchi wa china wanazaa watoto kulingana na agizo la dola nasio wanavyotaka wao!
Swala hilo nitofauti sana katika nchi nyingi za kiafrika mfano Tanzania, ambapo unaweza kuona familia moja ina karibu watoto sita, saba mpaka nane! Watoto hao huzaliwa kama ndege kwenye kiota na pindi wanapokuwa na kuota mabawa huruka huku na kule pasipokuzingatia suala la elimu au afya. Baadhi ya familia hizo huona fahari kubwa kwa kuwa na idadi kubwa ya watoto. Kama inavyofahamika bara la Afrika ndilo masikini zaidi duniani, lakini linaongoza kwa kuwa na kiwango cha juu katika kuzaa watoto. Matokeo yake ni kushindwa kuwapa watoto hao huduma kama vile SHULE na AFYA. Heeh! Watanzania wenzangu na Waafrika kwa ujumla amkeni! achaneni na dhana inayowaumiza. Mda umefika kwenda pamoja na mabadiliko ya dunia, tuachane na utaratibu au mazoea ya kale, tutakufa MASIKINI!?

Hebu tuliangalie bara la Ulaya, ambalo ndilo bara tajiri zaidi duniani. Chakushangaza zaidi hapa ni kwamba, idadi ya watu katika bara lote Ulaya haifikii ile ya nchi ya china! Hapa tunajifunza nini? Ikiwa Uingereza wana uwezo wa kiuchumi , mbona hawazaliani kama ilivyo kwa Tanzania? Si wazaliane tu kwa wingi, kwa kuwa wao wana uwezo wakuwatunza watoto wao? Je nchi hizi za Ulaya zinzingatia nini? Mbona zinakumbwa na uhaba wa wafanyakazi hata kudiriki kuwaingiza wafanyakazi toka nchi nyingine ?

Katika baadhi ya vitabu vya dini vimesisistiza kwamba, watu wakazaline na kuijaza dunia, na baadhi ya wanadini huoa wake zaidi ya mmoja jambo ambalo linatoa nafasi ya kuwa na watoto wengi katika familia na hatimaye nchi kwa ujumla.

Ndugu msomaji , uwanja ni wako, fungua masikio na macho yako tafuta pa kuegemea!

No comments: